JUMA LA KUMI NA MBILI
Tumeuitikia
mwaliko wa Yesu mpendwa wetu. Kwa kiwango fulani, tumeashiria utayari wetu wa kushirikiana na Yesu katika kazi
aliyotumwa kuifanya na Mungu Baba hapa duniani.
Ni pendo linaloendelea kukua ndani yetu, kati yetu na Yesu, na
tunaliacha liendelee kukua—tunaacha uhusiano wa kushirikiana na Kristu uendelee
kujengeka.
Tunapozidi
kukomaa katika kupenda hasa pale anayehusika ni aliyetutendea
mengi mazuri, tunakuwa na shauku kubwa sana ya kuwa na yule tunayempenda, na
pia kujua mengi iwezekanavyo kumhusu huyo tumpendaye. La kushangaza sana katika
kupenda, ni kuwa kila wakati inaonekana kuwa hatuwezi kujua yote tunayotaka
kumhusu tumpendaye. Kiu yetu ya kutaka kumjua tunayempenda haitoshelezwi hadi
mwisho.
Katika
juma hili na majuma yanayofuata, nia yetu moja ni kujua mengi iwezekanavyo
yanayomhusu Yesu Kristu. Bila shaka
tunatambua kujua huku tunakokutafuta si kwa akili
zetu tu; bali kwa kiasi kikubwa ni ya utambuzi wa ndani unaozidi kutujengea
ukaribu wa pekee na yule tumpendaye. Ukaribu huu unaendana na shauku ya kutaka kuwa naye wakati wote katika
utume wake. Hivyo basi tunaweza kusema nia yetu ni kumjua Kristu kwa ukamilifu zaidi,
ili tuweze kumpenda kwa undani zaidi, na upendo huu wa ndani zaidi utuongezee
uwezo wa kumfuasa kwa karibu zaidi.
Katika
siku za mwanzo za mafungo haya, tulijaribu kuangalia historia ya maisha yetu kwa
njia ya kujitafakari tukitazama kitabu
cha picha cha maisha yetu—kitabu chenye picha nyingi, zijulikanazo na
wengine na zingine tuzijuazo sisi wenyewe tu, picha zingine tuzioneazo aibu na
zingine zitupazo majigambo ya moyoni, zingine zenye kutupa simanzi na nyingine zenye
kutukumbusha furaha zilizopita tukiwa na wapendwa wetu... Sasa tunamwomba Yesu atuonyeshe Kitabu Chake cha Picha (“Photo Album”). Katika shauku yetu ya kujua mengi
yanayomhusu, tunamwomba Yesu Kristu asitufiche chochote—atuambie hadithi au
wasifu wote wa maisha yake ili kwamba tuweze kumpenda zaidi, yeye tunayetamani
kumjua kwa undani zaidi. Hakika kuna
thamani ya pekee kumjua yule anayetualika kumfuasa katika kutekeleza kazi
aliyotumwa na Baba Yake.
Juma
hili tunaanzia hapo mwanzoni. Tunamtafakari Mungu katika umilele wake, yaani hali yake ya kutokuwa na mwanzo wala
mwisho. Tunamtafakari Mungu katika Utatu
wake Mtakatifu kama vile akiutazama ulimwengu wetu kutoka juu mbinguni—akitazama matendo na wasifu wa binadamu wote, na
kujawa na huruma kiasi cha kumtuma mwanaye Yesu kuja kutukomboa. Hata sisi tukijaribu kutafakari kitabu cha
picha za vita vya dunia na vita vingine vingi, biashara ya utumwa, vifo
vitokanavyo na magojwa na njaa, mauaji ya kimbari katika sehemu mbalimbali,
athari za UKIMWI, chuki za kidini na kikabila n.k., tunaweza kuona wazi wasifu
wa mwanadamu ambao hakika unamgusa sana Mungu atupendaye kiasi cha kutuhurumia
sana. Picha tuliyopewa katika juma hili ni ya
Sarayevo, Boznia na Hesgovina ikionyesha uharibifu wa vita kati Juma
hili na tutumie yale tunayopewa kutusaidia kutafakari na kuingia ndani ya fumbo
la umwilisho wa Mungu katika Kristu na uamuzi wa Mungu kuukomboa
ulimwengu. Tayari tumekwishaona athari za
dhambi na kumuasi Mungu katika maisha yetu—si dhambi na uasi wa wanadamu kwa
ujumla wetu tu, bali pia katika uasi na udhambi wetu binafsi. Sasa tunatafakari mwitikio wa Mungu kwa
dhambi ya Zana za Kukusaidia Kuanza Juma Hili
Katika
maisha ya kila siku, kupata wa kumpenda hakuhitaji msaada wala juhudi nyingi. Ni kama vile jambo hutokea tu bila juhudi yoyote. Kwa tafakari ya moja kwa moja, wazungumzao Kiingereza wanasema
“kuangukia katika mapenzi”. Ni kama vile
jambo lisilopangwa, ni kwa bahati tu mtu “huanguka”, hivi basi inaonekana kuwa
ni jambo lenye urahisi wa kiajali,
japokuwa aangukaye aweza kuumia vibaya. Ni wazi kuwa kuangukia katika mapenzi hakuna kile vipengele muhimu ambavyo
kwavyo tunaweza kujifunza lolote la kutusaidia katika kupata kile hasa
tunachokitafuta katika majuma yaliyo mbele yetu. Vilevile, kama sote tujuavyo kutunza uhusiano
wa mapendo ya kweli huhusisha kujitolea mhanga ambako hakuwezi kufanyika bila
kuwepo kwa uaminifu wa hali ya juu kati ya wapendenao. Si suala la ajali tu, bali ni suala
linalohusisha nia na hisia zetu za ndani sana.
Tujaribu
tena kufikiria kuhusu hali ya kuanza kupenda. Ni nini hasa kinachoanzisha wawili kupendana? Ni nini tunachokitenda katika hatua za kwanza kabisa tujikutapo tumeanza kumpenda mtu fulani? Je huanza kwa kile tunachokiita kukutanishwa? Labda wakati mwingine ni “kukutanishwa” na
mtu ambaye ni mgeni kabisa katika maisha yetu. Kuna kitu fulani ambacho hutokea ndani yetu na tunajikuta katika hali
inayogusa na kunyanyua mioyo yetu kumwelekea tuanzaye kumpenda. Kiini cha hayo yote ni kuvutiwa sana na huyu tuliyekutanishwa naye, na tunagundua hali ya namna fulani ya kutaka kuwa pamoja naye. Kutokea
hapo, kuvutiwa kwetu na yule tunayempenda kunaongezeka na pia hali iliyo ngumu
kutawalika ya kutaka kuwa na yule tumpendaye wakati wote huongezeka kwa kiasi
kikubwa. Upendo unaokua hulisha na
kukuza shauku ya kukuza muungano—shauku ya kuwa na mpendwa wetu katika hali ya
undani wa hali ya juu. Mwanzoni hili
hutokea bila utambuzi wetu, ila kabla muda mrefu sana haujapita, tunapata
ufahamu kuwa tupo katika mapendo. Tunaanza kulifanyia kazi pendo
hilo. Tunakuwa na mawazo mengi yanayomhusu tunayempenda, na hata tukiwa
tunafanya kazi zetu za kawaida, tunakuwa na ndoto
za mchana zinazotuhusu sisi na tumpendaye. Tunamtembelea au kumpigia simu yule tunayempenda mara nyingi zaidi na
kupanga kuwa na muda mwingi zaidi pamoja. Tunakumbuka mazungumzo yetu yote, na wakati tukiwa hatuko na
tunayempenda tunayarudiarudia akilini mwetu—kama vile kucheza tena na tena muziki
tunaoupenda. Mwanzoni tunajikuta
tukizungumza na tunayempenda kuhusiana na yote na chochole. Hakuna lolote linalomhusu tumpendaye linaloweza
kuleta mazungumzo yasiyovutia au yenye uchoshi. Tunapenda kujua yote yanayohusu maisha ya tunayempenda; aliyopitia
maishani, jinsi
alivyofanya uchaguzi mbalimbali maishani, yale anayopenda na yale asiyopenda na
yapi hasa yanamfanya kuwa alivyo. Tunagundua mengi mapya kumhusu tunayempenda, na katika kila ugunduzi,
tunajikuta mwunganiko wetu wa ki-mapendo ukiongezeka. Tunatafuta njia za kuonyesha mapendo yetu kwa
tumpendaye: tunajaribu kutumia maneno mororo, tunatumia matendo yanayojali, na
kufanya mengi yanayoonyesha kujitolea ili kumfanya mwenzetu awe mwenye furaha
na faraja. Kila neno tumsemezalo na tendo tumtendealo tunayempenda huchangia
katika kukua kwa pendo letu. Hatusahau
daima ishara ya kwanza kabisa aliyotuonyesha kuwa anatupenda. Kwa kadiri upendo wetu unavyokua, ndivyo
hivyo pia kiwango cha wajibu wetu katika pendo hili kinavyoongezeka—najikuta
nikitafuta kitu cha kunihakikishia kuwa nimpendaye atukuwa nami katika
maisha. Kwa upande wangu naonyesha kuwa
nitawajibika na kujitoea mhanga katika hali yoyote ili pendo letu liendelee.
Kama
haya yamepata kukutokea kwa namna yoyote ulipopenda katika maisha yako, au kama
yanakumbushia yale yaliyotokea katika kupenda, basi yatakuwa ya msaada mkubwa
katika majuma yanayofuata. Tupo katika
mwelekeo wa kuanza kumpenda Yesu. Tunaweza kujaribu kuhisi hatua ya kwanza ambayo ni kukutanishwa kwetu na Kristu. Tunaweza kujipa muda wa kushuhudia jinsi shauku yetu ya kuwa na Yesu
inavyoongezeka, ikisababisha kujiwa na maswali mengi, ikitufanya tutunge misemo
mingi ya kuelezea mapendo yetu kwa Yesu, na kuonyesha dhamira ya kuwa naye
pamoja wakati wote.
Huu
ni msaada wa kutenda na si wa kufikiri wala si
zoezi la kupata elimu ya kutusaidia kuangalia “Kitabu cha Picha cha
Yesu”. Hili ni suala la moyoni. Kufikia kiwango hiki katika mafungo yetu,
tayari tumeunganika na Yesu ndani mioyoni mwetu. Sasa tuna nia ya kuyapa nafasi mapendo haya
yaongezeke kina.
Kurasa
za mwanzo za Kitabu cha Picha cha Maisha ya Yesu kinaturudisha “hapo mwanzo”, na kutuweka katika
tafakari ya taswira bunifu ya Jumuiya ya Utatu Mtakatifu ikiuangalia ulimwengu
wa binadamu kutoka juu mbinguni, na kujawa na huruma moyoni.
Tafakari
ya huruma ya Mungu Baba katika kumtuma Yesu Kristu katika ulimwengu wetu
na katika maisha yetu inaweza kuwa na mguso wa pekee katika mioyo yetu. Jinsi tunavyozidi kutafakari, kwa mfano mauaji
ya Bosnia au yale ya kimbari ya Rwanda ambayo yanaigusa pia huruma ya Mungu
katika Kristu, ndivyo tunavyozidi kumtambua Yesu ni nani. Ukweli kuwa Yesu yu kwa ajili yetu unashinda
upeo wetu wa udhanifu na utambuzi. Umwilisho wa Yesu hakika washinda elimu yote na uwezo wote wa mwanadamu
wa kuelewa. Yesu Kristu, Mungu kamili
anajishusha na kujiweka katika hali duni kiasi hicho! Hakika hakuna tena sehemu ya maisha yangu
ambayo naweza kusema niko peke yangu.
Katika
juma hili lote, fanya zoezi la kurudia kusema maneno haya: “Bwana, nisaidie kukujua kikamilifu, ili
niweze kukupenda kwa dhati zaidi, ili kwamba niwe nawe kikamilifu zadi.” Vilevile unaweza kupenda kuimba kila siku
wimbo wowote unaotumia maneno haya ya Mt. Inyasi wa Loyola: “Ee Bwana wangu, mambo matatu nakuomba:
kukuona wewe kwa udhahiri zaidi; kukupenda wewe kwa dhati zaidi; na kukufuasa
kwa ukaribu zaidi—siku baada ya siku.”
Kabla
ya kulala kila siku, naweza kujiwekea muda mfupi wa kujiuliza ni neno gani nadhani
linafaa nimwambie Yesu ninayempenda. Bila shaka muda huu mfupi utakuwa pia muda wa kuburudishwa na furaha na
faraja ya ndani inayonijia nilipotambua jinsi pendo langu na kuvutiwa kwangu na
Yesu kunavyoongezeka.
Kwa Ajili ya Safari: Ishara za Mungu
Nguvu
za kuvutiwa kwa yuke tunayempenda huanza kufanya kazi pale tumpendaye anapotoa
ishara kwa maneno au kwa matendo. Kwa
kawaida kila mmoja huvutiwa kutaka kujua maana ya ishara fulani ili aweze
kuiitikia inavyostahili. Watu hutoa
ishara mbalimbali kwa kutumia karibu viungo Mungu
alifanya majaribio mengi ya kuvutia usikivu na hisia zetu kwa ujumla wake kwa
kupitia maagano mbalimbali na wahenga wetu wa Kiyahudi. Ishara hizi zilianza na kundelea kwa karne
nyingi—zikawa kama vile Mungu kuwa katika wakati
wa uchumba mrefu jamii ya wanadamu. Sasa tunashuhudia kilele cha ishara za Mungu kwa Katika Maneno Haya au Mengine Yanayofanana Nayo...
Ee
Bwana,
Unajisikiaje
ukiuangalia kutoka juu mbinguni ulimwengu
uliouumba? Hakika unaona kupendeza
kwake, kupendeza kwa mali asili zake, watu wanaojaliana, watoto wakizaliwa n.k. Lakini nina hakika kuwa kuna hali nyingine ya
ulimwengu unayoiona, hali ya mabaya: watoto wakishinda njaa na wengine wakifa kwa njaa na magojwa katika
mikono ya mama zao; silaha zikipewa uzito kuliko watu ambao zimeundwa kuwalinda; watu wachovu na wapweke
wakizurura mitaani, wakiwa hawana kazi, makazi wala kujaliwa na wengine kama
binadamu...
Kutoka
katika starehe ya nyumba yangu salama, najaribu kuiangalia picha ya juma hili—Picha
ya athari za vita. Naona nyumba
zilizopigwa mabomu, moshi ukipanda juu, maua madogo yamesalia katika
miti... Mara inabadika kutoka kama picha
ya sehemu iliyo katika vita na kuwa picha ya sehemu ya mtaa wangu. Kama katika mtaa wangu, watu katika nyumba
hizo zilizoteketea walikuwa katika hali yao ya kawaida. Kutoka katika nyumba hizi watu waliondoka
kwenda kazini, wengine kusherehekea matukio ya kifamilia, wakizungumzia mipango
ya harusi na kujadiliana kuhusu vitabu na masomo, wakiazima unga kutoka kwa
jirani zao, kwa furaha watoto wakicheza na kuimba nyimbo nzuri za kitoto...
Sasa yote yamepotea katika magofu yanayoteketea kwa moto. Mtaa wangu si tofauti, waweza kuwa kama huu
wa Sarayevo.
Unauangaliaje
ulimwengu kama huo ambapo tunauana na kubomoleana nyumba; ambapo tunatiliana Lakini
katika tendo lisiloelezeka wala kufikirika la mapendo, huruma yako inakufanya
kujitoa kikamilfu kwa ulimwengu uliouumba. Kwa njia ya ajabu sana unatuonyesha tena ni kwa kiasi gani
unatupenda—unakuja na kuwa mmoja wetu. Ee Bwana, inawezekanaje kutupenda sisi kiasi hicho, sisi tunaoonyesha
chuki kila siku kwa maneno na matendo yetu? Tena umetenda hili ukijua wazi kuwa hili litahusisha maumivu ya hali ya
juu kwako, litakusababishia mahangaiko mengi unapojitahidi kutuonyesha kuwa
bado tunapendeka na tunatupendwa na
Mungu, na zaidi ukijua kuwa kujitoa kwako kuwa mwanadamu kunahusisha kifo?
Ee Bwana,
nifundishe kupenda zaidi. Nakuomba,
tafadhali nipe nafasi nione na kuhisi jinsi gani uliishi maisha yako hapa duniani. Natamani kukujua zaidi na nataka kuwa nawe
hapa duniani. Natamani kukubali mwaliko
wako: kukupa NDIYO yangu. Nikubali niwe
rafiki wako unapotembea hapa duniani. Niruhusu nijifuze kutoka kwako jinsi ya kuwa vile Mungu alivyoniumba
niwe; zungumza na unieleze jinsi ya kuwa mwanadamu mwenye utu ulioniumbia, utu
nilioupoteza kwa kutenda maovu, lakini unanirudishia, iwapo nipo tayari
kuupokea kwa njia ya umwilisho
wako. Nipe uwezo wa kuyapanga maisha
yangu yashabihiane na yako.
Tazama
nayastahi sana mapendo yako kwa wanadamu—mapendo yako kwangu. Kwa kiasi fulani yananipa
hisia ya ajabu moyoni—yananitisha kwa kuwa siyastahili; ila sijisikii kukimbia
bali kuyajia na kuyakumbatia, kwa kuwa wewe mwenyewe unanistahilisha. Mapendo yako yananivutia—nipe neema yako ili
mapendo yako yaniumbie moyo unaofanana na wako Mtakatifu. Naishiwa maneno ya kukwambia—niseme nini
zaidi mbele ya mapendo haya? Ee Yesu
nasema “asante sana” japokuwa najua asante yangu haielezei kikamilifu shukrani niliyonayo. Nishike mkono Bwana. Zungumza nami. Nionyeshe tena kitabu cha picha za maisha yako. Nisaidie kukwambia “ndiyo” kila siku.
Maandiko Matakatifu
Waefesi
1:3-14
Wakolosai 1:9-22
Yohana 1:1-18 |
MAFUNGO YA KIROHO KUPITIA MTANDAO