JUMA LA KUMI NA NNE
Mungu Anatangaza Njia; Watumishi Wako Tayari
Mwongozo: Imani ya Watu Alimozaliwa Yesu
Tunapoangalia albamu ya picha ya rafiki yetu,
baadhi ya picha zinazotuvutia zaidi ni zile za wazazi na za bibi na babu zake. Tunajaribu kuziangalia picha hizo kwa ukaribu
na umakini zaidi ili kuona jinsi ambavyo rafiki yetu anaweza kuwa amefanana na
mama, baba, bibi au babu wake. Tunajaribu pia kuchunguza iwapo kuna ushabihiano wowote wa tabia, sifa na
mienendo ya nafsi, kati ya rafiki yetu na wahenga wake—jinsi walivyosimama
kupiga picha, mavazi waliyonayo, shughuli waliyokuwa wakifanya pichani, ishara
za usoni, nk.
Katika juma hili tutatumia sura za kwanza ya
Injili ya Matayo na ya Luka katika kufuatilia matamanio yetu yanaoongezeka daima
ya kumjua Yesu kwa ukamilifu zaidi, ili kwamba tuweze kumpenda kwa undani
zaidi, kwa sababu tunataka kumfuasa kwa uhuru zaidi.
Mbinu au utaratibu wetu juma hili utakuwa “kukodolea
macho” nyuso za Zakaria na Elizabeti, Yosefu na Maria (Mariamu), ili kuona ni
nini wanatuambia kuhusu mpendwa wetu Yesu. Tutajaribu kujipenyeza katika matukio kadhaa ya Biblia huku tukiendelea
na shughuli zetu za maisha na kazi za kila siku. Tutajaribu kujua zaidi kuhusu tabia na sifa
za nafsi ya Yesu. Hii tutafanya kwa
kupitia njia ya kujielewesha kwanza imani ya jamii alimokulia ambayo ilikuwa na
ushawishi mkubwa katika kumjengea tabia na utu wake kwa ujumla.
Mtindo huu wa kusali unahitaji mazoezi, ila mtu
yeyote anaweza kuyafanya, kwa sababu ni jambo ambalo tunalifanya bila kukusudia
kila tunapokutana na wazazi wa tumpendaye. Na tujapojua jambo fulani kuhusu
familia ya rafiki yetu, inakuwa ni kama kujua jambo kujifunza jambo moja zaidi
kumhusu rafiki yetu. Kwa msaada zaidi
kuhusu namna hii ya kusali hakikisha umesoma na kuelewa zana za kukusaidia
kusali unazopewa.
Zakaria hakuweza kuwaza ni jinsi gani Mungu
angeweza kupata ushindi mbele ya uzee wa mkewe Elizabeti—wangewezaje kupata
motto katika uzee huo? Hakuweza
kuzungumza lolote hadi ilipofikia wakati wa kutamka jina la mtoto wao wa kiume,
“Mungu ni Mwaminifu”. Malaika alimwarifu
Maria kuwa “...kwa Mungu hakuna
lisilo wezekana.’’ Elizabeti anasema, “Wewe umebarikiwa kwa kuwa uliamini kwamba Bwana atatimiza
yale aliyokuambia.” Nafsi yote ya
Maria inatangaza ukuu wa Mungu, na maneno na mwenendo wake vinatamka wazi imani
ya wahenga wake.
Tunapoendelea na shughuli zetu za maisha kila
siku, hadithi hizi zenye maajabu ya kupendeza zitalipa juma letu sura
maalum. Atakuwepo Zakaria wakati
tunapokuwa na mashaka, pale ambapo tunapotilia mashaka hata uwepo wa
Mungu. Muda mwingine wa
mashaka-ya-Zakaria pale tunapoweza hatimaye kusema, “Mungu ni Mwaminifu”. Kutakuwa na muda ambapo picha ya wiki hii
katika kompyuta yetu itatukumbusha hisia za nzito na kusema, “Hii
itawezekanaje?” Na utafika muda ambapo picha hiyo itakukumbusha maneno ya
Maria, “Mini ni Mtumishi wa Bwana, nitendewe ulivyosema.”
Zana za Kukusaidia Kuanza Juma Hili
Alipokuwa akimwongoza kiroho mtu mwenye tamaa yake
ya kumjua, kumpenda na kumfuasa Yesu, Mt. Inyasi wa Loyola aliwamfundisha
kutafakari matukio mbalimbali katika Injili, akitilia mkazo zaidi suala ya
kuwekwa huru. Katika juma hili na majuma
mengine yanayofuata, tutajifunza kufanya hivi katika namna inayoendana vema
zaidi na maisha yetu ya shughuli kila siku.
Baada ya kusoma simulizi fulani ya tukio katika
Injili, tunaweza kuliwaza na kuwa na picha ya wazi kabisa ya yale
yaliyotokea. Lakini hii si toauti sana
na mtu kutusimulia kwa uwazi tukio katika maisha yake. Ni kweli kuwa kuna thamani katika simulizi
hizi, lakini kuna mbinu nyingine yenye kuingia ndani kabisa ya tukio, na
inawezekana kwa kuwa Maandiko Matakatifu ni Neno la Mungu. Hadithi au simulizi hizi ni ufunuo wa Mungu
ulio hai na ufanyao kazi. Hivyo basi,
tunaposoma Injili, kuna jambo linalotokea ndani ya mioyo yetu. Ufunuo wa Mungu unakwenda mbele zaidi na hata kupita mahali andiko tulilosoma
lilipoishia.
Mtakatifu Inyasi anatuhamasisha kuingia ndani au kupenya ndani ya simulizi ya tukio. Hataki tusikilize tu, na kupata ukweli wa lile lililotokea. Ananitaka mimi nilipenye tukio hilo, liwe na maana katika maisha yangu na kunipa ufunuo
wa Mungu—zoezi hili hufanyika zaidi ndani moyoni na si akilini tu. Namna hii ya kutafakari hunipeleka ndani
zaidi ya Neno la Mungu kuliko simulizi tu ya Neno hilo, ambayo inaweza kusomwa
na yeyote ajuaye kusoma au kusikiliza, na kuwaza kwa akili yake. Nikisoma Neno la Mungu kwa moyo namna hiyo, Neno hilo linakuwa hai
ndani yangu na Yesu huzungumza nami ndani
moyoni, na nakuwa mshiriki hai katika
tukio husika. Hebu tujaribu kuchukua mifano
miwili.
Kipindi cha Sala ya Kutafakari Tukio Katika
Injili
Kama nina muda, kati ya dakika thelathini hadi
arobaini na tano, naweza kupata mengi sana kutoka katika tukio lolote katika
Injili. Nitaanza kwa kujiweka binafsi
mbele ya Mungu. Kisha, rasmi nitamweleza Mungu ni neema ipi hasa ninayohitaji
kutoka kwake katika muda wa sala. Kwa
mfano nia yangu yaweza kuwa ‘kuelewa kwa undani zaidi Yesu ni nani, ili kwamba
mapenzi yangu kwake yaongezeke, na nitamani zaidi kuwa naye.’
Kisha nitasoma kutoka katika Injili, simulizi ya
tukio husika na kuiweka Biblia pembeni. Taratibu nitaanza kufanya taswira au picha ya lile lililotokea kwa
ukamilifu niwezavyo. Tukio linatokea
wapi? Tambua na tilia maanani vyote
vilivyopo katika tukio na vinavyolizunguka tukio. Ni nani yuko hapo? Waaliopo wamevaa mavazi gani? Hali ya hewa,
ni joto au baridi kiasi gani? Harufu
gani naweza kunusa? Napenyeza katika
tukio ndani zaidi kwa kuwa mmojawapo katika tukio. Naweza kuwa mmojawapo katika kundi kubwa la
watu, au naweza kuwa mmojawapo wa watu wanaotajwa kwa majina katika tukio. Ninapofikia hapo naliwacha tukio liendelee
kutendeka, na kwenda popote linaponipeleka. Nikiwa nimelipenyeza tukio na kuwa sehemu yake, maneno na matendo ni
zaidi ya mfano mkanda wa video wa tukio unaochezwa tena. Kutoka ndani ya tukio, naweza kurudi nyuma na kulipa tukio mtazamo mpya. Kwa mfano, naweza kutoa nafasi yale
niliyofunuliwa yafanywe katika maneno, matendo na ishara za wale wanaohusika
katika tukio, au naweza kutulia na kutilia maanani yale yanayotokea moyoni
mwangu. Maelezo ya tukio yanapungua
umuhimu kwa kuwa tukio lenyewe limeingia moyoni mwangu—si jambo lililo nje bali
ni jambo lililo sasa sehemu ya matukio katika maisha yangu. Mwishowe namaliza kwa sala, nikizungumza na
Mungu wangu ndani moyoni, yeye kama rafiki ninayempenda sana wala sio Bwana
ninayemwogopa—nitamweleza lolote linalonijia moyoni, nikimpa shukrani kwa neema
nilizopokea muda mfupi uliopita.
Kutafakari Tukio la Katika Maisha ya Kila Siku
Kuna mambo mengi ambayo hutufanya tusiwe huru hapa
duniani—mengine yamesababishwa na jamii na tamaduni zetu, udhaifu wa kibinadamu
unaohitaji msaada wa Mungu, na kikubwa zaidi udhambi wetu binafsi au udhambi wa
jamii.
Tukiwa na mtazamo wa uhuru, yawezekana kutumia
simulizi ya Neno la Mungu kuzaa matunda hata tukiwa katika harakati za maisha
yetu ya kila siku. Katika juma hii, kwa
mfano, nitaamka asubuhi, na wakati nikijiweka tayari kuanza siku yangu
(nikinawa au kuoga, nikichana nywele, kuvaa nguo nk.), nitakuwa nikifikiria juu
ya matukio katika Biblia ambayo tutatafakari juma hili. Juma hili litakuwa juu ya Yosefu, Zakaria,
Elizabeti na Mariamu. Kisha nitajaribu
kujikumbusha kwa kifupi habari zilizopo katika masomo yanayowahusu hao (kumbuka
tunatumia Sura za kwanza za Injili ya Luka na ya Matayo). Hapa yaweza kuwa kama hivi: jitihada ya
kuamini kuwa hakuna lishindikanalo kwa Mungu, kujikakamua katika kuipokea hali ya
kulazimika kumtegemea Mungu na kuishi katika imani, kujiweka wazi kufunuliwa
ukweli wa uaminifu wa Mungu. Kisha nitaipitia
akilini siku iliyo mbele yangu. Nikiwa
katika hali ya moyo wazi, kunaweza kutokea mashahibiano, mlingano au muungano
katika ya Neno ninalotafakari na matukio katika siku yangu, au kumbukumbu ya
maisha yangu inayonijia.
Yaweza kuwa kuna mivutano katika ndoa yangu na ni
vigumu kwangu kuamini kuwa uaminifu wa Mungu kwetu una nguvu kuliko ukaidi wetu. Katika mfano huu, ninapokuwa na mwenzangu wa
ndoa, naweza kuona jinsi hali yangu inavyoweza kuwa na ushahibiano wake na
simulizi za Injili zinazomhusu Zakaria na Maria—wakati mmoja nikijikuta siwezi
kusema lolote hadi ninapoweza kutamka, “Mungu ni Mwaminifu,” au wakati mwingine
kujisalimisha kwa Mungu “Mimi ni Mtumishi wako Bwana.” Au nikimsikia Elizabeti akisema, “Mwenyezi
Mungu amekubariki, kwa sababu uliamini kuwa atatimiza ahadi zake.”
Labda yote ninayotarajia ni mzunguko wa kawaida wa
shughuli nyingi za kazi za kila siku, zilizojaa harakati na shinikizo nyingi
ambazo nazitekeleza katika hali ya kawaida. Katika majuma yaliyopita ya mafungo
haya, niligundua kuwa shughuli na mahangaiko yangu ya kila siku yaweza kuwa sehemu
ya hali ya udhaifu na udhambi wangu, na pia sehemu ya upendo mkuu wa Mungu
unaoshinda udhaifu na udhambi wangu kabisa. Juma hili laweza kuwa na mazao mengi sana ya kiroho iwapo nitapitia
maisha yangu kama vile mtu anayekagua shamba kake, nitatazama kwa makini
matukio mbalimbali katika maisha yangu, kama vile Elizabeti. Jaribu kuwa na maswali kama haya daima moyoni
unapoyapitia maisha yako: “imekuwa kama hivi kwa muda mrefu kiasi kwamba
sitegemei badiliko lolote?”; “Mimi ni nani hadi kudhani nitawahi kuzaa matunda
kuliko niwezavyo?”, “Katika uzee huu, hali
hii ya ukimya wa tumbo langu la uzazi kuwa kama aliyelaaniwa, yawezekana
mimi kudhani naweza kuzaa sauti iitayo jangwani, ‘Tayarisheni njia ya Bwana’?”
Labda kuingia katika uwanja wa matukio ya maisha yangu ya kila siku ni kukariri mstari
mmoja kutoka katika simulizi ya Injili na kuuacha upenye moyo wangu ninapousema
nikiwa hata na pumziko fupi kama vile kungojea usafiri, kuwa katika foleni
katika dirisha la huduma nk.—nitaurudia mara nyingi iwezekanavyo, huku nikiwa
natambua ninachofanya na kutokusahau kuwa ninasema Neno la Mungu. Mfano mzuri juma hili ni kurudia maneno ya
Mariamu, “Moyo wangu wote wamtukuza Bwana” au “Mwenyezi Mungu amenitazama
mtumishi wake mnyonge.”
Mwishowe, itakuwa vema kama utajaribu
kuwashirikisha wengine tafakari hizi, mbinu ulizotumia na neema
ulizopokea. Unaweza kufanya hivi kwa
kutembelea katika mtandao huu Sehemu ya
Kushirikishana iliyo katika Ukurasa wa Mwongozo.
Kwa Ajili ya Safari: Kutumia Udhanifu Katika Sala
“Dunia imejawa na nishati tukufu ya Mungu.” Padre
Mjezuiti na mshairi Gerard Manley Hopins anapiga mbiu hii yenye maana mbili
katika mstari wa kwanza wa shairi lake mashuhuri kuhusu ulimwengu wetu
unaopendwa na Mungu
Ulimwengu una msukumo unaoendeshwa kama vile kwa nishati
kubwa ya umeme ili kudhihirisha utukufu wa Mungu. Ulimwengu pia una nishati kama ya umeme
inayosukuma kutenda jambo fulani lililo muhimu sana. Maana zote mbili zimezingatiwa katika juma hili.
Kwa mfano, tukiangalia kile kilichokuwa kinawasukuma kwa ndani Elizabeti, Mariamu
na mwanamume aitwaye Yosefu ni nishati ishindayo uwezo wao wa kibinadamu.
Inahitaji aina fulani ya unyeyekevu ili kushangaa—unyenyekevu
unaotoa nafasi kutendeka lisilotarajiwa, lisilo la kawawaida au hata
linalotisha. Aina hii ya unyenyekevu
tunaweza pia kuiita “uwazi”. Ni hali ya msimamo au silika ya ndani moyoni inayompa mtu hali ya kuwa tayari kutokupinga
au kupokea lolote linaloweza kusemwa au kupewa. Si hali ambayo mtu anakuwa nayo sasa na kuipoteza baada ya muda mfupi,
au inabagua lini kuwa wazi na lini kutokuwa wazi. Ni hali ya moyo inayodumu
hivyo basi kumpa mtu mtazamo usiotetereka, na kuwa na hali ya kuguswa na
yanayotokea au kuwa na hisia hai isiyosinzia-sinzia kuelekea matukio mbalimbali,
huku na kule.
Tunasali tukiwa na neema hii ya
unyenyekevu na tukiomba kupewa neema hii zaidi juma hili tunapowatazama
Elizabeti, Mariamu na Yosefu wakitekeleza nafasi zao katika mpango wa wokovu
wetu. Ni kama tupo katika aya za awali
za sura ya mwisho ya Historia ya Wokovu
Wetu. Hapa tutaanza kumjua Yesu na
namna yake ya kuishi na kuwaza. Kama ni
igizo jukwani, basi Yesu ni anaonekana hapa kama “mwigizaji mkuu” na wengine
kama waigizaji wanaotekeleza nafasi zao ambazo ni za kumleta “mwigizaji mkuu”
jukwaani.
Mtakatifu Inyasi anasisitiza wale
wanaofanya Mazoezi ya Kiroho kujaribu kupenyeza tukio au simulizi husika kwa
kutumia uwezo wao wa kutafakari. Mara
nyingi tunatumia kumbumbu na uwezo wetu wa kufikiri na kusahau zawadi kubwa
tuliyopewa kwa asili, uwezo wa kutafakari. Tumeshawishika tunaweza kuufikia ukweli kwa urahisi zaidi kwa kupitia
mantiki, utumiaji wa takwimu na kumbukumbu, hivyo basi kuzarau umuhimu wa
kutafakari—tunasema kutafakari kunazaa ‘ndoto za mchana’ zisizo na umuhimu
wowote maishani.
Saikolojia (Elimu Nafsia) inatumia mlango
wa fahamu wa kutazama ili kuanzisha tafakari ambayo tunaijua kama vile ‘vipimo
vya upachikaji’ (projective tests). Labda umewahi kutumia kipimo cha Rorscharch; Katika kipimo hicho unaonyeshwa michoro na
madoa anuwai ya wino, na kwa kutumia yale utakayosema baada ya kuyaangalia madoa
hayo, mambo kadhaa ya kweli kukuhusu yanakuwa wazi kwa yule anayekupa kipimo
hicho. Mpimaji kapata ukweli kwa kutumia
tafakari. Tafakari ina uwezo na nguvu
kubwa kuliko wengi tunavyoamini. Mtakatifu Inyasi aliamini kuwa zawadi zote alizopewa mtu: kusikia,
kusema, kuelewa, kujieleza, kukumbuka, kuona, kuhisi, kufikiri, kuwaza,
kutafakari, kutaamuli nk., zinaweza kutumiwa na Mungu kutujia au kuwasiliana
nasi.
Juma hili basi na tutumie zawadi hii ya kutafakari
ili tuwe tayari kupokea neema ya uwazi, unyenyekevu na matumaini. Jitahidi kuwa macho kujua umesimama wapi
wakati Mariamu anapotokewa na malaika. Usisahau kile unachodhani malaika anamwambia Mariamu na ni kipi Mariamu
anawaza..unasema nini na unafanya nini unampomfuatilia Mariamu kwenda nyumbani
kwa Elizabeti? Ni kipi Yosefu anafanya
anapoamka baada ya ndoto ambapo anatambua inampasa kumuoa Mariamu mchumba wake
japokuwa ana ujauzito usio wake?
Baada ya hapo Mtakatifu Inyasi anasihi kufanya tafakari
kutuhusu sisi ili tuweze kupata mang’amuzi na neema kutoka katika zoezi
hili. Labda tunaweza kumtazama Mariamu
kwa umbali, hivyo ni vema. Sasa na
tusali tukiwa na hizo hisia za kuwa mbali naye. Pengine umbali umekuja kutokana ja kutotaka kuwa na lolote linalohusu
sehemu hiyo, na hapa basi tunapata mwito wa kuomba imani zaidi. Sasa tupo hapa, tumeuweka ukweli katika sala,
ukweli ambao uhalisi wake umefumbuliwa katika hali mpya na ya kushangaza. Kwa Mt. Inyasi, kuwa karibu na Yesu na rafiki
zake wa karibu ni kuwa karibu na sisi wenyewe, kuwa karibu na nafsi zetu. Hili si suala la kujipenda kibinafsi au kujitenga
kichoyo. Hili linasababishwa na ukweli
kuwa kwa kadiri ninavyokuwa karibu na nafsi yangu na karibu na ukweli halisi
kunihusu, ndivyo naweza kutambua ukaribu wa kimapendo kwangu ambao Yesu
anao. Umwilisho wa Ukweli wa Mungu
unaingia katika maisha ya hawa watu watatu kwa ‘kuwa-nishati-sha’ kwa imani na kuwapa neema ya uwazi na unyenyekevu
wa kupokea vema ajabu na mshangao huo wa ujio wa Yesu. Juma hili linatisha, ila
pia linatuliwaza hasa pale tunapojionea jitihada za mwanadamu kutoa nafasi kwa
Mungu katika sehemu ambayo amekuwa akiamini kwa muda mrefu ni yake binafsi,
nafasi ya faragha. Tunasali kwamba nasi
tupokee nishati ya uwepo mtukufu wa Mungu.
Katika Maneno Haya au Mengine Yanayofanana Nayo...
Yesu Mpendwa,
Asante kwa kunionyesha tena albabu ya picha za
jamaa yako yako. Kuna utofauti kidogo
kusali kwa namna hii, na naweza kujihisi nikiwa na utambuzi zaidi wa nafsi
yangu. Kuwa nami katika hili. Ipe nafasi hali hii inilete karibu zaidi
nawe.
Namtazama Elizabeti na Zakria wakifanya juhudi za
kila namna ili kupata uzao, na kisha wanakata tamaa. Hakika lilikuwa jambo zito zana! Je, walikaa
pamoja wakaikumbatika pamoja hii ‘bahati mbaya’? Waliweza kuibeba vipi hali yao hii katika
maisha yao ya ndoa? Halafu, miaka mingi
imepita, wakati Elizabeti anakuwa mkongwe, malaika anawatokea na kuwaeleza kuwa
watapata mtoto wa kiume.
Kisha nawatazama Mariamu na Yosefu—Mariamu akiwa
bado mwanamwali. Namwona akicheka
jikoni, huku akitayarisha supu katika jiko, akiwafurahisha rafiki zake kwa
hadithi za kuchekesha. Bwana Yesu, ni
kutoka kwake huyu atakayekuwa mama yako ndiyo ulijifunza kusimulia hadithi? Kisha namuona mwanamwali huyu mchangamfu
mwenye kicheko kinachovutia, kasimama jikoni akiwa pekee wakati malaika
anapomtokea. “Atakuwa Mama wa Mungu?” Natazama kwa mshangao anapokakamkia habari hii. Anajua wazi habari hii itayageuza maisha yake
kabisa—mambo hayatakuwa tena kama alivyotarajia! Je, yupo radhi kuacha maisha yake
kuchangamanishwa namna hii? Alitaka na
kutegemea maisha ya kawaida tu: kuwapikia rafiki zake, kufunga ndoa na Yusufu,
na kwenda katika Sinagogi kusali kila wiki. Ni kweli kuwa alitaka kuishi maisha yake yote akikuamini na kukutumainia
Mungu wake, lakini ilikuwa sharti iwe katika hali ngumu namna hii?
Sikutegemea Mariamu angekusumbua moyoni. Nilifikiria kuwa ulitabasamu tu kitakatiffu
na uamuzi ulikamilika. Lakini sasa namwona
akikakamkia woga wake na kusali akimwomba Mungu kama ilivyokuwa kawaida yake
alipoogopa jambo fulani. Woga wake unayeyuka. Kama hivi ndivyo Mungu atakavyo maisha yake
yawe, yupo tayari kuyaishi. Namwona tena, bado kasimama jikoni, supu bado inachemka
katika jiko. Anageuka na kwa taaratibu
anamtazama malaika usoni na kusema, “Ndiyo.”
Nguvu ya sala hii mbele zako inanishangaza, ee
Yesu. Namwangalia mama yako na namwona
akiwa mtu wa kawaida mbele yangu. Namwona akisema “Ndiyo” yake. Napata tena kujikumbusha kuwa nipo katika sala halisi na si katika
ndoto. Labda uwezo wangu wa kutafakari
unanyong’onyea. Nafanya kile alichofanya
Mariamu. Nipo katika hali ya kuogopa,
hivyo namsalia Mungu. Taratibu woga
unapungua.
Sikumbuki kama nimewahi kumwona Mama yako katika
hali ya uhalisi wa kibinadamu namna hii—akiwa hai machoni pangu, mtu wa kawaida
mwenye kufurahi, anayepata mashaka na anayesali kama yeyote anayemwamini
Mungu. Namwona akisema ‘ndiyo’ yake, na hii inanikumbusha ‘ndiyo’ yangu katika maisha yangu. Nataka kukujua zaidi na kufanya maisha yangu
yafanane zaidi na ya kwako. Nataka kuwa
wazi kupokea ujumbe wowote unaonitumia, japokuwa najua wajumbe wako hawatanijia
katika umbo la malaika wenye mbawa. Najua ujumbe wako utanifikia kwa kupitia watu ninaowaona na kuwa nao
kila siku katika maisha yangu. Yesu
wangu, nisaidie kumtambua yule umtumaye kuniletea ujumbe. Nisaidie kuusikiliza na kuuelewa ujumbe; na
zaidi ya yote, nipe moyo niweze kusema “Ndiyo”.
Maandiko Matakatifu:
Luka 1:5-25, 57-66
Luka 1:26-38
Luka 1:39-56
Luka 1:67-79
Matayo 1:
18-24
|
MAFUNGO YA KIROHO KUPITIA MTANDAO